Surah 78: An-Naba — النبأ
عَمَّ يَتَسَآءَلُونَ
WANAULIZANA nini?
عَنِ ٱلنَّبَإِ ٱلْعَظِيمِ
Ile khabari kuu,
ٱلَّذِى هُمْ فِيهِ مُخْتَلِفُونَ
Ambayo kwayo wanakhitalifiana.
كَلَّا سَيَعْلَمُونَ
La! Karibu watakuja jua.
ثُمَّ كَلَّا سَيَعْلَمُونَ
Tena la! Karibu watakuja jua.
أَلَمْ نَجْعَلِ ٱلْأَرْضَ مِهَٰدًۭا
Kwani hatukuifanya ardhi kama tandiko?
وَٱلْجِبَالَ أَوْتَادًۭا
Na milima kama vigingi?
وَخَلَقْنَٰكُمْ أَزْوَٰجًۭا
Na tukakuumbeni kwa jozi?
وَجَعَلْنَا نَوْمَكُمْ سُبَاتًۭا
Na tukakufanya kulala kwenu ni mapumziko?
وَجَعَلْنَا ٱلَّيْلَ لِبَاسًۭا
Na tukaufanya usiku ni nguo?
وَجَعَلْنَا ٱلنَّهَارَ مَعَاشًۭا
Na tukaufanya mchana ni wa kuchumia maisha?
وَبَنَيْنَا فَوْقَكُمْ سَبْعًۭا شِدَادًۭا
Na tukajenga juu yenu saba zenye nguvu?
وَجَعَلْنَا سِرَاجًۭا وَهَّاجًۭا
Na tukaifanya taa yenye mwanga na joto;
وَأَنزَلْنَا مِنَ ٱلْمُعْصِرَٰتِ مَآءًۭ ثَجَّاجًۭا
Na tukateremsha maji yanayo anguka kwa kasi kutoka mawinguni,
لِّنُخْرِجَ بِهِۦ حَبًّۭا وَنَبَاتًۭا
Ili tutoe kwayo nafaka na mimea,
وَجَنَّٰتٍ أَلْفَافًا
Na mabustani yenye miti iliyo kamatana.
إِنَّ يَوْمَ ٱلْفَصْلِ كَانَ مِيقَٰتًۭا
Hakika siku ya uamuzi imewekewa wakati wake,
يَوْمَ يُنفَخُ فِى ٱلصُّورِ فَتَأْتُونَ أَفْوَاجًۭا
Siku litapo pulizwa barugumu, nanyi mtakuja kwa makundi,
وَفُتِحَتِ ٱلسَّمَآءُ فَكَانَتْ أَبْوَٰبًۭا
Na mbingu zitafunguliwa, ziwe milango,
وَسُيِّرَتِ ٱلْجِبَالُ فَكَانَتْ سَرَابًا
Na milima itaondolewa na itakuwa kama sarabi.
إِنَّ جَهَنَّمَ كَانَتْ مِرْصَادًۭا
Hakika Jahannamu inangojea!
لِّلطَّٰغِينَ مَـَٔابًۭا
Kwa walio asi ndio makaazi yao,
لَّٰبِثِينَ فِيهَآ أَحْقَابًۭا
Wakae humo karne baada ya karne,
لَّا يَذُوقُونَ فِيهَا بَرْدًۭا وَلَا شَرَابًا
Hawataonja humo chochote kibaridi wala kinywaji,
إِلَّا حَمِيمًۭا وَغَسَّاقًۭا
Ila maji yamoto sana na usaha,
جَزَآءًۭ وِفَاقًا
Ndio jaza muwafaka.
إِنَّهُمْ كَانُوا۟ لَا يَرْجُونَ حِسَابًۭا
Hakika hao hawakuwa wakitaraji kuwa kuna hisabu.
وَكَذَّبُوا۟ بِـَٔايَٰتِنَا كِذَّابًۭا
Na wakikanusha Aya zetu kwa nguvu.
وَكُلَّ شَىْءٍ أَحْصَيْنَٰهُ كِتَٰبًۭا
Na kila kitu Sisi tumekidhibiti kwa kukiandika.
فَذُوقُوا۟ فَلَن نَّزِيدَكُمْ إِلَّا عَذَابًا
Basi onjeni! Nasi hatutakuzidishieni ila adhabu!
إِنَّ لِلْمُتَّقِينَ مَفَازًا
Hakika wachamngu wanastahiki kufuzu,
حَدَآئِقَ وَأَعْنَٰبًۭا
Mabustani na mizabibu,
وَكَوَاعِبَ أَتْرَابًۭا
Na wake walio lingana nao,
وَكَأْسًۭا دِهَاقًۭا
Na bilauri zilizo jaa,
لَّا يَسْمَعُونَ فِيهَا لَغْوًۭا وَلَا كِذَّٰبًۭا
Hawatasikia humo upuuzi wala uwongo -
جَزَآءًۭ مِّن رَّبِّكَ عَطَآءً حِسَابًۭا
Malipo kutoka kwa Mola wako Mlezi, kipawa cha kutosha.
رَّبِّ ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلْأَرْضِ وَمَا بَيْنَهُمَا ٱلرَّحْمَٰنِ ۖ لَا يَمْلِكُونَ مِنْهُ خِطَابًۭا
Mola Mlezi wa mbingu na ardhi na vilio baina yao, Arrahman, Mwingi wa rehema; hawamiliki usemi mbele yake!
يَوْمَ يَقُومُ ٱلرُّوحُ وَٱلْمَلَٰٓئِكَةُ صَفًّۭا ۖ لَّا يَتَكَلَّمُونَ إِلَّا مَنْ أَذِنَ لَهُ ٱلرَّحْمَٰنُ وَقَالَ صَوَابًۭا
Siku atakapo simama Roho na Malaika kwa safu. Hawatasema ila Mwingi wa rehema aliye mruhusu, na atasema yaliyo sawa tu.
ذَٰلِكَ ٱلْيَوْمُ ٱلْحَقُّ ۖ فَمَن شَآءَ ٱتَّخَذَ إِلَىٰ رَبِّهِۦ مَـَٔابًا
Hiyo ndiyo Siku ya haki. Basi anaye taka na ashike njia arejee kwa Mola wake Mlezi.
إِنَّآ أَنذَرْنَٰكُمْ عَذَابًۭا قَرِيبًۭا يَوْمَ يَنظُرُ ٱلْمَرْءُ مَا قَدَّمَتْ يَدَاهُ وَيَقُولُ ٱلْكَافِرُ يَٰلَيْتَنِى كُنتُ تُرَٰبًۢا
Hakika tumekuhadharisheni adhabu iliyo karibu kufika; Siku ambayo mtu atakapo ona yaliyo tangulizwa na mikono yake; na kafiri atasema: Laiti ningeli kuwa udongo!
Surah 79: An-Naziat — النازعات
وَٱلنَّٰزِعَٰتِ غَرْقًۭا
Naapa kwa wanao komoa kwa nguvu,
وَٱلنَّٰشِطَٰتِ نَشْطًۭا
Na kwa wanao toa kwa upole,
وَٱلسَّٰبِحَٰتِ سَبْحًۭا
Na wanao ogelea,
فَٱلسَّٰبِقَٰتِ سَبْقًۭا
Wakishindana mbio,
فَٱلْمُدَبِّرَٰتِ أَمْرًۭا
Wakidabiri mambo.
يَوْمَ تَرْجُفُ ٱلرَّاجِفَةُ
Siku kitapo tetemeka cha kutetemeka,
تَتْبَعُهَا ٱلرَّادِفَةُ
Kifuate cha kufuatia.
قُلُوبٌۭ يَوْمَئِذٍۢ وَاجِفَةٌ
Siku hiyo nyoyo zitapiga piga,
أَبْصَٰرُهَا خَٰشِعَةٌۭ
Macho yatainama chini.
يَقُولُونَ أَءِنَّا لَمَرْدُودُونَ فِى ٱلْحَافِرَةِ
Sasa wanasema: Ati kweli tutarudishwa kwenye hali ya kwanza?
أَءِذَا كُنَّا عِظَٰمًۭا نَّخِرَةًۭ
Hata tukiwa mifupa iliyo bunguliwa?
قَالُوا۟ تِلْكَ إِذًۭا كَرَّةٌ خَاسِرَةٌۭ
Wanasema: Basi marejeo hayo ni yenye khasara!
فَإِنَّمَا هِىَ زَجْرَةٌۭ وَٰحِدَةٌۭ
Kwa hakika hayo ni ukelele mmoja tu,
فَإِذَا هُم بِٱلسَّاهِرَةِ
Mara watakuwa kwenye uwanda wa mkutano!
هَلْ أَتَىٰكَ حَدِيثُ مُوسَىٰٓ
Je! Imekufikia hadithi ya Musa?
إِذْ نَادَىٰهُ رَبُّهُۥ بِٱلْوَادِ ٱلْمُقَدَّسِ طُوًى
Mola wake Mlezi alipo mwita katika bonde takatifu la T'uwaa, akamwambia:
ٱذْهَبْ إِلَىٰ فِرْعَوْنَ إِنَّهُۥ طَغَىٰ
Nenda kwa Firauni. Hakika yeye amezidi jeuri.
فَقُلْ هَل لَّكَ إِلَىٰٓ أَن تَزَكَّىٰ
Umwambie: Je! Unapenda kujitakasa?
وَأَهْدِيَكَ إِلَىٰ رَبِّكَ فَتَخْشَىٰ
Nami nitakuongoa ufike kwa Mola wako Mlezi, upate kumcha.
فَأَرَىٰهُ ٱلْءَايَةَ ٱلْكُبْرَىٰ
Basi alimwonyesha Ishara kubwa.
فَكَذَّبَ وَعَصَىٰ
Lakini aliikadhibisha na akaasi.
ثُمَّ أَدْبَرَ يَسْعَىٰ
Kisha alirudi nyuma, akaingia kufanya juhudi.
فَحَشَرَ فَنَادَىٰ
Akakusanya watu akanadi.
فَقَالَ أَنَا۠ رَبُّكُمُ ٱلْأَعْلَىٰ
Akasema: Mimi ndiye Mola wenu Mlezi mkuu kabisa.
فَأَخَذَهُ ٱللَّهُ نَكَالَ ٱلْءَاخِرَةِ وَٱلْأُولَىٰٓ
Basi hapo Mwenyezi Mungu akamshika kumuadhibu kwa la mwisho na la mwanzo.
إِنَّ فِى ذَٰلِكَ لَعِبْرَةًۭ لِّمَن يَخْشَىٰٓ
Kwa hakika katika haya yapo mazingatio kwa wanao ogopa.
ءَأَنتُمْ أَشَدُّ خَلْقًا أَمِ ٱلسَّمَآءُ ۚ بَنَىٰهَا
Je! Ni vigumu zaidi kukuumbeni nyinyi au mbingu? Yeye ndiye aliye ijenga!
رَفَعَ سَمْكَهَا فَسَوَّىٰهَا
Akainua kimo chake, na akaitengeneza vizuri.
وَأَغْطَشَ لَيْلَهَا وَأَخْرَجَ ضُحَىٰهَا
Na akautia giza usiku wake, na akautokeza mchana wake.
وَٱلْأَرْضَ بَعْدَ ذَٰلِكَ دَحَىٰهَآ
Na juu ya hivyo ameitandaza ardhi.
أَخْرَجَ مِنْهَا مَآءَهَا وَمَرْعَىٰهَا
Akatoa ndani yake maji yake na malisho yake,
وَٱلْجِبَالَ أَرْسَىٰهَا
Na milima akaisimamisha,
مَتَٰعًۭا لَّكُمْ وَلِأَنْعَٰمِكُمْ
Kwa nafuu yenu na mifugo yenu.
فَإِذَا جَآءَتِ ٱلطَّآمَّةُ ٱلْكُبْرَىٰ
Basi itakapo fika hiyo balaa kubwa,
يَوْمَ يَتَذَكَّرُ ٱلْإِنسَٰنُ مَا سَعَىٰ
Siku ambayo mtu atakumbuka aliyo yafanya,
وَبُرِّزَتِ ٱلْجَحِيمُ لِمَن يَرَىٰ
Na Jahannamu itadhihirishwa kwa mwenye kuona,
فَأَمَّا مَن طَغَىٰ
Basi ama yule aliye zidi ujeuri,
وَءَاثَرَ ٱلْحَيَوٰةَ ٱلدُّنْيَا
Na akakhiari maisha ya dunia,
فَإِنَّ ٱلْجَحِيمَ هِىَ ٱلْمَأْوَىٰ
Kwa hakika Jahannamu ndiyo makaazi yake!
وَأَمَّا مَنْ خَافَ مَقَامَ رَبِّهِۦ وَنَهَى ٱلنَّفْسَ عَنِ ٱلْهَوَىٰ
Na ama yule anaye ogopa kusimamishwa mbele ya Mola wake Mlezi, na akajizuilia nafsi yake na matamanio,
فَإِنَّ ٱلْجَنَّةَ هِىَ ٱلْمَأْوَىٰ
Basi huyo, Pepo itakuwa ndiyo makaazi yake!
يَسْـَٔلُونَكَ عَنِ ٱلسَّاعَةِ أَيَّانَ مُرْسَىٰهَا
Wanakuuliza Saa (ya Kiyama) itakuwa lini?
فِيمَ أَنتَ مِن ذِكْرَىٰهَآ
Una nini wewe hata uitaje?
إِلَىٰ رَبِّكَ مُنتَهَىٰهَآ
Kwa Mola wako Mlezi ndio mwisho wake.
إِنَّمَآ أَنتَ مُنذِرُ مَن يَخْشَىٰهَا
Kwa hakika wewe ni mwonyaji tu kwa mwenye kuikhofu.
كَأَنَّهُمْ يَوْمَ يَرَوْنَهَا لَمْ يَلْبَثُوٓا۟ إِلَّا عَشِيَّةً أَوْ ضُحَىٰهَا
Ni kama kwamba wao siku watapo iona (hiyo Saa) hawakukaa ila jioni moja tu, au mchana wake.
Surah 80: Abasa — عبس
عَبَسَ وَتَوَلَّىٰٓ
Alikunja kipaji na akageuka,
أَن جَآءَهُ ٱلْأَعْمَىٰ
Kwa sababu alimjia kipofu!
وَمَا يُدْرِيكَ لَعَلَّهُۥ يَزَّكَّىٰٓ
Na nini kitakujuulisha pengine yeye atatakasika?
أَوْ يَذَّكَّرُ فَتَنفَعَهُ ٱلذِّكْرَىٰٓ
Au atawaidhika, na mawaidha yamfae?
أَمَّا مَنِ ٱسْتَغْنَىٰ
Ama ajionaye hana haja,
فَأَنتَ لَهُۥ تَصَدَّىٰ
Wewe ndio unamshughulikia?
وَمَا عَلَيْكَ أَلَّا يَزَّكَّىٰ
Na si juu yako kama hakutakasika.
وَأَمَّا مَن جَآءَكَ يَسْعَىٰ
Ama anaye kujia kwa juhudi,
وَهُوَ يَخْشَىٰ
Naye anaogopa,
فَأَنتَ عَنْهُ تَلَهَّىٰ
Ndio wewe unampuuza?
كَلَّآ إِنَّهَا تَذْكِرَةٌۭ
Sivyo hivyo! Huku ni kukumbushana.
فَمَن شَآءَ ذَكَرَهُۥ
Basi anaye penda akumbuke.
فِى صُحُفٍۢ مُّكَرَّمَةٍۢ
Yamo katika kurasa zilizo hishimiwa,
مَّرْفُوعَةٍۢ مُّطَهَّرَةٍۭ
Zilizo inuliwa, zilizo takaswa.
بِأَيْدِى سَفَرَةٍۢ
Zimo mikononi mwa Malaika waandishi,
كِرَامٍۭ بَرَرَةٍۢ
Watukufu, wema.
قُتِلَ ٱلْإِنسَٰنُ مَآ أَكْفَرَهُۥ
Ameangamia mwanaadamu! Nini kinacho mkufurisha?
مِنْ أَىِّ شَىْءٍ خَلَقَهُۥ
Kwa kitu gani amemuumba?
مِن نُّطْفَةٍ خَلَقَهُۥ فَقَدَّرَهُۥ
Kwa tone la manii, akamuumba na akamkadiria.
ثُمَّ ٱلسَّبِيلَ يَسَّرَهُۥ
Kisha akamsahilishia njia.
ثُمَّ أَمَاتَهُۥ فَأَقْبَرَهُۥ
Kisha akamfisha, akamtia kaburini.
ثُمَّ إِذَا شَآءَ أَنشَرَهُۥ
Kisha apendapo atamfufua.
كَلَّا لَمَّا يَقْضِ مَآ أَمَرَهُۥ
La! Hajamaliza aliyo muamuru.
فَلْيَنظُرِ ٱلْإِنسَٰنُ إِلَىٰ طَعَامِهِۦٓ
Hebu mtu na atazame chakula chake.
أَنَّا صَبَبْنَا ٱلْمَآءَ صَبًّۭا
Hakika Sisi tumemimina maji kwa nguvu,
ثُمَّ شَقَقْنَا ٱلْأَرْضَ شَقًّۭا
Tena tukaipasua pasua ardhi kwa nguvu,
فَأَنۢبَتْنَا فِيهَا حَبًّۭا
Kisha tukaotesha humo nafaka,
وَعِنَبًۭا وَقَضْبًۭا
Na zabibu, na mimea ya majani,
وَزَيْتُونًۭا وَنَخْلًۭا
Na mizaituni, na mitende,
وَحَدَآئِقَ غُلْبًۭا
Na bustani zenye miti iliyo songana baraabara,
وَفَٰكِهَةًۭ وَأَبًّۭا
Na matunda, na malisho ya wanyama;
مَّتَٰعًۭا لَّكُمْ وَلِأَنْعَٰمِكُمْ
Kwa manufaa yenu na mifugo yenu.
فَإِذَا جَآءَتِ ٱلصَّآخَّةُ
Basi utakapo kuja ukelele,
يَوْمَ يَفِرُّ ٱلْمَرْءُ مِنْ أَخِيهِ
Siku ambayo mtu atamkimbia nduguye,
وَأُمِّهِۦ وَأَبِيهِ
Na mamaye na babaye,
وَصَٰحِبَتِهِۦ وَبَنِيهِ
Na mkewe na wanawe -
لِكُلِّ ٱمْرِئٍۢ مِّنْهُمْ يَوْمَئِذٍۢ شَأْنٌۭ يُغْنِيهِ
Kila mtu miongoni mwao siku hiyo atakuwa na lake la kumtosha.
وُجُوهٌۭ يَوْمَئِذٍۢ مُّسْفِرَةٌۭ
Siku hiyo ziko nyuso zitazo nawiri,
ضَاحِكَةٌۭ مُّسْتَبْشِرَةٌۭ
Zitacheka, zitachangamka;
وَوُجُوهٌۭ يَوْمَئِذٍ عَلَيْهَا غَبَرَةٌۭ
Na nyuso siku hiyo zitakuwa na mavumbi,
تَرْهَقُهَا قَتَرَةٌ
Giza totoro litazifunika,
أُو۟لَٰٓئِكَ هُمُ ٱلْكَفَرَةُ ٱلْفَجَرَةُ
Hao ndio makafiri watenda maovu.
Surah 81: At-Takwir — التكوير
إِذَا ٱلشَّمْسُ كُوِّرَتْ
Jua litakapo kunjwa,
وَإِذَا ٱلنُّجُومُ ٱنكَدَرَتْ
Na nyota zikazimwa,
وَإِذَا ٱلْجِبَالُ سُيِّرَتْ
Na milima ikaondolewa,
وَإِذَا ٱلْعِشَارُ عُطِّلَتْ
Na ngamia wenye mimba pevu watakapo achwa wasishughulikiwe,
وَإِذَا ٱلْوُحُوشُ حُشِرَتْ
Na wanyama wa mwituni wakakusanywa,
وَإِذَا ٱلْبِحَارُ سُجِّرَتْ
Na bahari zikawaka moto,
وَإِذَا ٱلنُّفُوسُ زُوِّجَتْ
Na nafsi zikaunganishwa,
وَإِذَا ٱلْمَوْءُۥدَةُ سُئِلَتْ
Na msichana aliye zikwa hai atapo ulizwa,
بِأَىِّ ذَنۢبٍۢ قُتِلَتْ
Kwa kosa gani aliuliwa?
وَإِذَا ٱلصُّحُفُ نُشِرَتْ
Na madaftari yatakapo enezwa,
وَإِذَا ٱلسَّمَآءُ كُشِطَتْ
Na mbingu itapo tanduliwa,
وَإِذَا ٱلْجَحِيمُ سُعِّرَتْ
Na Jahannamu itapo chochewa,
وَإِذَا ٱلْجَنَّةُ أُزْلِفَتْ
Na Pepo ikasogezwa,
عَلِمَتْ نَفْسٌۭ مَّآ أَحْضَرَتْ
Kila nafsi itajua ilicho kihudhurisha.
فَلَآ أُقْسِمُ بِٱلْخُنَّسِ
Naapa kwa nyota zinapo rejea nyuma,
ٱلْجَوَارِ ٱلْكُنَّسِ
Zinazo kwenda, kisha zikajificha,
وَٱلَّيْلِ إِذَا عَسْعَسَ
Na kwa usiku unapo pungua,
وَٱلصُّبْحِ إِذَا تَنَفَّسَ
Na kwa asubuhi inapo pambazuka,
إِنَّهُۥ لَقَوْلُ رَسُولٍۢ كَرِيمٍۢ
Kwamba hakika bila ya shaka hii ni kauli ya Mjumbe mtukufu,
ذِى قُوَّةٍ عِندَ ذِى ٱلْعَرْشِ مَكِينٍۢ
Mwenye nguvu na mwenye cheo kwa huyo Mwenye Kiti cha Enzi,
مُّطَاعٍۢ ثَمَّ أَمِينٍۢ
Anaye t'iiwa, tena muaminifu.
وَمَا صَاحِبُكُم بِمَجْنُونٍۢ
Na wala huyu mwenzenu hana wazimu.
وَلَقَدْ رَءَاهُ بِٱلْأُفُقِ ٱلْمُبِينِ
Na hakika yeye alimwona kwenye upeo wa macho ulio safi.
وَمَا هُوَ عَلَى ٱلْغَيْبِ بِضَنِينٍۢ
Wala yeye si bakhili kwa mambo ya ghaibu.
وَمَا هُوَ بِقَوْلِ شَيْطَٰنٍۢ رَّجِيمٍۢ
Wala hii si kauli ya Shetani maluuni.
فَأَيْنَ تَذْهَبُونَ
Basi mnakwenda wapi?
إِنْ هُوَ إِلَّا ذِكْرٌۭ لِّلْعَٰلَمِينَ
Haikuwa hii ila ni ukumbusho kwa walimwengu wote.
لِمَن شَآءَ مِنكُمْ أَن يَسْتَقِيمَ
Kwa yule miongoni mwenu anaye taka kwenda sawa.
وَمَا تَشَآءُونَ إِلَّآ أَن يَشَآءَ ٱللَّهُ رَبُّ ٱلْعَٰلَمِينَ
Wala nyinyi hamtataka isipo kuwa atake Mwenyezi Mungu Mola Mlezi wa walimwengu wote.
Surah 82: Al-Infitar — الإنفطار
إِذَا ٱلسَّمَآءُ ٱنفَطَرَتْ
Mbingu itapo chanika,
وَإِذَا ٱلْكَوَاكِبُ ٱنتَثَرَتْ
Na nyota zitapo tawanyika,
وَإِذَا ٱلْبِحَارُ فُجِّرَتْ
Na bahari zitakapo pasuliwa,
وَإِذَا ٱلْقُبُورُ بُعْثِرَتْ
Na makaburi yatapo fukuliwa,
عَلِمَتْ نَفْسٌۭ مَّا قَدَّمَتْ وَأَخَّرَتْ
Hapo kila nafsi itajua ilicho tanguliza, na ilicho bakisha nyuma.
يَٰٓأَيُّهَا ٱلْإِنسَٰنُ مَا غَرَّكَ بِرَبِّكَ ٱلْكَرِيمِ
Ewe mwanaadamu! Nini kilicho kughuri ukamwacha Mola wako Mlezi Mtukufu?
ٱلَّذِى خَلَقَكَ فَسَوَّىٰكَ فَعَدَلَكَ
Aliye kuumba, akakuweka sawa, akakunyoosha,
فِىٓ أَىِّ صُورَةٍۢ مَّا شَآءَ رَكَّبَكَ
Katika sura yoyote aliyo ipenda akakujenga.
كَلَّا بَلْ تُكَذِّبُونَ بِٱلدِّينِ
Sivyo hivyo! Bali nyinyi mnaikanusha Siku ya Malipo.
وَإِنَّ عَلَيْكُمْ لَحَٰفِظِينَ
Na hakika bila ya shaka wapo walinzi juu yenu,
كِرَامًۭا كَٰتِبِينَ
Waandishi wenye hishima,
يَعْلَمُونَ مَا تَفْعَلُونَ
Wanayajua mnayo yatenda.
إِنَّ ٱلْأَبْرَارَ لَفِى نَعِيمٍۢ
Hakika wema bila ya shaka watakuwa katika neema,
وَإِنَّ ٱلْفُجَّارَ لَفِى جَحِيمٍۢ
Na hakika waovu bila ya shaka watakuwa Motoni;
يَصْلَوْنَهَا يَوْمَ ٱلدِّينِ
Wataingia humo Siku ya Malipo.
وَمَا هُمْ عَنْهَا بِغَآئِبِينَ
Na hawatoacha kuwamo humo.
وَمَآ أَدْرَىٰكَ مَا يَوْمُ ٱلدِّينِ
Na nini kitakacho kujuulisha Siku ya Malipo ni siku gani?
ثُمَّ مَآ أَدْرَىٰكَ مَا يَوْمُ ٱلدِّينِ
Tena nini kitakacho kujuulisha Siku ya Malipo ni siku gani?
يَوْمَ لَا تَمْلِكُ نَفْسٌۭ لِّنَفْسٍۢ شَيْـًۭٔا ۖ وَٱلْأَمْرُ يَوْمَئِذٍۢ لِّلَّهِ
Siku ambayo nafsi haitakuwa na madaraka yoyote juu ya nafsi; na amri yote siku hiyo ni ya Mwenyezi Mungu tu.
Surah 83: Al-Mutaffifin — المطففين
وَيْلٌۭ لِّلْمُطَفِّفِينَ
Ole wao hao wapunjao!
ٱلَّذِينَ إِذَا ٱكْتَالُوا۟ عَلَى ٱلنَّاسِ يَسْتَوْفُونَ
Ambao wanapo jipimia kwa watu hudai watimiziwe.
وَإِذَا كَالُوهُمْ أَو وَّزَنُوهُمْ يُخْسِرُونَ
Na wao wanapo wapimia watu kwa kipimo au mizani hupunguza.
أَلَا يَظُنُّ أُو۟لَٰٓئِكَ أَنَّهُم مَّبْعُوثُونَ
Kwani hawadhani hao kwamba watafufuliwa
لِيَوْمٍ عَظِيمٍۢ
Katika Siku iliyo kuu,
يَوْمَ يَقُومُ ٱلنَّاسُ لِرَبِّ ٱلْعَٰلَمِينَ
Siku watapo msimamia watu Mola Mlezi wa walimwengu wote?
كَلَّآ إِنَّ كِتَٰبَ ٱلْفُجَّارِ لَفِى سِجِّينٍۢ
Hasha! Hakika maandiko ya wakosefu bila ya shaka yamo katika Sijjin.
وَمَآ أَدْرَىٰكَ مَا سِجِّينٌۭ
Unajua nini Sijjin?
كِتَٰبٌۭ مَّرْقُومٌۭ
Kitabu kilicho andikwa.
وَيْلٌۭ يَوْمَئِذٍۢ لِّلْمُكَذِّبِينَ
Ole wao siku hiyo kwa wanao kadhibisha!
ٱلَّذِينَ يُكَذِّبُونَ بِيَوْمِ ٱلدِّينِ
Ambao wanaikadhibisha Siku ya Malipo.
وَمَا يُكَذِّبُ بِهِۦٓ إِلَّا كُلُّ مُعْتَدٍ أَثِيمٍ
Wala haikadhibishi ila kila mwenye kuruka mipaka, mwenye dhambi.
إِذَا تُتْلَىٰ عَلَيْهِ ءَايَٰتُنَا قَالَ أَسَٰطِيرُ ٱلْأَوَّلِينَ
Anapo somewa Aya zetu husema: Ni visa vya watu wa kale!
كَلَّا ۖ بَلْ ۜ رَانَ عَلَىٰ قُلُوبِهِم مَّا كَانُوا۟ يَكْسِبُونَ
Hasha! Bali yametia kutu juu ya nyoyo zao hao walio kuwa wakiyachuma.
كَلَّآ إِنَّهُمْ عَن رَّبِّهِمْ يَوْمَئِذٍۢ لَّمَحْجُوبُونَ
Hasha! Hakika hao siku hiyo bila ya shaka watazuiliwa na neema za Mola wao Mlezi.
ثُمَّ إِنَّهُمْ لَصَالُوا۟ ٱلْجَحِيمِ
Kisha wataingia Motoni!
ثُمَّ يُقَالُ هَٰذَا ٱلَّذِى كُنتُم بِهِۦ تُكَذِّبُونَ
Kisha waambiwe: Haya ndiyo mliyo kuwa mkiyakadhabisha.
كَلَّآ إِنَّ كِتَٰبَ ٱلْأَبْرَارِ لَفِى عِلِّيِّينَ
Hasha! Hakika maandiko ya watu wema bila ya shaka yamo katika I'liyyin.
وَمَآ أَدْرَىٰكَ مَا عِلِّيُّونَ
Na nini kitakacho kujuvya nini I'liyyin?
كِتَٰبٌۭ مَّرْقُومٌۭ
Kitabu kilicho andikwa.
يَشْهَدُهُ ٱلْمُقَرَّبُونَ
Wanakishuhudia walio karibishwa.
إِنَّ ٱلْأَبْرَارَ لَفِى نَعِيمٍ
Hakika watu wema bila ya shaka watakuwa katika neema.
عَلَى ٱلْأَرَآئِكِ يَنظُرُونَ
Wakae juu ya viti vya enzi wakiangalia.
تَعْرِفُ فِى وُجُوهِهِمْ نَضْرَةَ ٱلنَّعِيمِ
Utatambua katika nyuso zao mng'aro wa neema,
يُسْقَوْنَ مِن رَّحِيقٍۢ مَّخْتُومٍ
Watanyweshwa kinywaji safi kiliyo tiwa muhuri,
خِتَٰمُهُۥ مِسْكٌۭ ۚ وَفِى ذَٰلِكَ فَلْيَتَنَافَسِ ٱلْمُتَنَٰفِسُونَ
Muhuri wake ni miski. Na katika hayo washindanie wenye kushindana.
وَمِزَاجُهُۥ مِن تَسْنِيمٍ
Na mchanganyiko wake ni Tasniim,
عَيْنًۭا يَشْرَبُ بِهَا ٱلْمُقَرَّبُونَ
Chemchem watakayo inywa walio kurubishwa.
إِنَّ ٱلَّذِينَ أَجْرَمُوا۟ كَانُوا۟ مِنَ ٱلَّذِينَ ءَامَنُوا۟ يَضْحَكُونَ
Kwa hakika wale walio kuwa wakosefu walikuwa wakiwacheka walio amini.
وَإِذَا مَرُّوا۟ بِهِمْ يَتَغَامَزُونَ
Na wanapo pita karibu yao wakikonyezana.
وَإِذَا ٱنقَلَبُوٓا۟ إِلَىٰٓ أَهْلِهِمُ ٱنقَلَبُوا۟ فَكِهِينَ
Na wanapo rudi kwa watu wao hurudi nao wamefurahi.
وَإِذَا رَأَوْهُمْ قَالُوٓا۟ إِنَّ هَٰٓؤُلَآءِ لَضَآلُّونَ
Na wanapo waona husema: Hakika hawa ndio khasa walio potea.
وَمَآ أُرْسِلُوا۟ عَلَيْهِمْ حَٰفِظِينَ
Na wao hawakutumwa wawe walinzi juu yao.
فَٱلْيَوْمَ ٱلَّذِينَ ءَامَنُوا۟ مِنَ ٱلْكُفَّارِ يَضْحَكُونَ
Basi leo walio amini ndio watawacheka makafiri,
عَلَى ٱلْأَرَآئِكِ يَنظُرُونَ
Nao wako juu ya viti vya enzi wakiangalia.
هَلْ ثُوِّبَ ٱلْكُفَّارُ مَا كَانُوا۟ يَفْعَلُونَ
Je! makafiri wamelipwa malipo ya yale waliyo kuwa wakiyatenda?
Surah 84: Al-Inshiqaq — الإنشقاق
إِذَا ٱلسَّمَآءُ ٱنشَقَّتْ
Itapo chanika mbingu,
وَأَذِنَتْ لِرَبِّهَا وَحُقَّتْ
Na ikamsikiliza Mola wake Mlezi, na ikapasiwa kumsikiliza,
وَإِذَا ٱلْأَرْضُ مُدَّتْ
Na ardhi itakapo tanuliwa,
وَأَلْقَتْ مَا فِيهَا وَتَخَلَّتْ
Na kuvitoa vilivyo kuwa ndani yake, ikawa tupu,
وَأَذِنَتْ لِرَبِّهَا وَحُقَّتْ
Na ikamsikiliza Mola wake Mlezi, na ikapasiwa kumsikiliza,
يَٰٓأَيُّهَا ٱلْإِنسَٰنُ إِنَّكَ كَادِحٌ إِلَىٰ رَبِّكَ كَدْحًۭا فَمُلَٰقِيهِ
Ewe mtu! Hakika wewe unajikusuru kwa juhudi kumwendea Mola wako Mlezi, basi utamkuta.
فَأَمَّا مَنْ أُوتِىَ كِتَٰبَهُۥ بِيَمِينِهِۦ
Ama atakaye pewa daftari lake kwa mkono wa kulia,
فَسَوْفَ يُحَاسَبُ حِسَابًۭا يَسِيرًۭا
Basi huyo atahisabiwa hisabu nyepesi,
وَيَنقَلِبُ إِلَىٰٓ أَهْلِهِۦ مَسْرُورًۭا
Na arudi kwa ahali zake na furaha.
وَأَمَّا مَنْ أُوتِىَ كِتَٰبَهُۥ وَرَآءَ ظَهْرِهِۦ
Na ama atakaye pewa daftari lake kwa nyuma ya mgongo wake,
فَسَوْفَ يَدْعُوا۟ ثُبُورًۭا
Basi huyo ataomba kuteketea.
وَيَصْلَىٰ سَعِيرًا
Na ataingia Motoni.
إِنَّهُۥ كَانَ فِىٓ أَهْلِهِۦ مَسْرُورًا
Hakika alikuwa furahani kati ya jamaa zake.
إِنَّهُۥ ظَنَّ أَن لَّن يَحُورَ
Huyo hakika alidhani kuwa hatarejea tena.
بَلَىٰٓ إِنَّ رَبَّهُۥ كَانَ بِهِۦ بَصِيرًۭا
Kwani? Hakika Mola wake Mlezi alikuwa akimwona!
فَلَآ أُقْسِمُ بِٱلشَّفَقِ
Basi ninaapa kwa wekundu wa jua linapo kuchwa,
وَٱلَّيْلِ وَمَا وَسَقَ
Na kwa usiku na unavyo vikusanya,
وَٱلْقَمَرِ إِذَا ٱتَّسَقَ
Na kwa mwezi unapo pevuka,
لَتَرْكَبُنَّ طَبَقًا عَن طَبَقٍۢ
Lazima mtapanda t'abaka kwa t'abaka!
فَمَا لَهُمْ لَا يُؤْمِنُونَ
Basi wana nini hawaamini?
وَإِذَا قُرِئَ عَلَيْهِمُ ٱلْقُرْءَانُ لَا يَسْجُدُونَ ۩
Na wanapo somewa Qur'ani hawasujudu?
بَلِ ٱلَّذِينَ كَفَرُوا۟ يُكَذِّبُونَ
Bali walio kufuru wanakanusha tu.
وَٱللَّهُ أَعْلَمُ بِمَا يُوعُونَ
Na Mwenyezi Mungu anajua wanayo yadhamiria.
فَبَشِّرْهُم بِعَذَابٍ أَلِيمٍ
Basi wabashirie adhabu chungu!
إِلَّا ٱلَّذِينَ ءَامَنُوا۟ وَعَمِلُوا۟ ٱلصَّٰلِحَٰتِ لَهُمْ أَجْرٌ غَيْرُ مَمْنُونٍۭ
Isipo kuwa wale walio amini na wakatenda mema; hao watakuwa na ujira usio malizika.
Surah 85: Al-Buruj — البروج
وَٱلسَّمَآءِ ذَاتِ ٱلْبُرُوجِ
Naapa kwa mbingu yenye Buruji!
وَٱلْيَوْمِ ٱلْمَوْعُودِ
Na kwa siku iliyo ahidiwa!
وَشَاهِدٍۢ وَمَشْهُودٍۢ
Na kwa shahidi na kinacho shuhudiwa!
قُتِلَ أَصْحَٰبُ ٱلْأُخْدُودِ
Wameangamizwa watu wa makhandaki
ٱلنَّارِ ذَاتِ ٱلْوَقُودِ
Yenye moto wenye kuni nyingi,
إِذْ هُمْ عَلَيْهَا قُعُودٌۭ
Walipo kuwa wamekaa hapo,
وَهُمْ عَلَىٰ مَا يَفْعَلُونَ بِٱلْمُؤْمِنِينَ شُهُودٌۭ
Na wao ni mashahidi wa yale waliyo kuwa wakiwafanyia Waumini.
وَمَا نَقَمُوا۟ مِنْهُمْ إِلَّآ أَن يُؤْمِنُوا۟ بِٱللَّهِ ٱلْعَزِيزِ ٱلْحَمِيدِ
Nao hawakuona baya lolote kwao ila kuwa wakimuamini Mwenyezi Mungu, Mwenye nguvu, Msifiwa,
ٱلَّذِى لَهُۥ مُلْكُ ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلْأَرْضِ ۚ وَٱللَّهُ عَلَىٰ كُلِّ شَىْءٍۢ شَهِيدٌ
Ambaye anao ufalme wa mbingu na ardhi; na Mwenyezi Mungu ni shaahidi wa kila kitu.
إِنَّ ٱلَّذِينَ فَتَنُوا۟ ٱلْمُؤْمِنِينَ وَٱلْمُؤْمِنَٰتِ ثُمَّ لَمْ يَتُوبُوا۟ فَلَهُمْ عَذَابُ جَهَنَّمَ وَلَهُمْ عَذَابُ ٱلْحَرِيقِ
Hakika walio wafitini Waumini wanaume na Waumini wanawake, kisha hawakutubu, basi watapata adhabu ya Jahannamu na watapata adhabu ya kuungua.
إِنَّ ٱلَّذِينَ ءَامَنُوا۟ وَعَمِلُوا۟ ٱلصَّٰلِحَٰتِ لَهُمْ جَنَّٰتٌۭ تَجْرِى مِن تَحْتِهَا ٱلْأَنْهَٰرُ ۚ ذَٰلِكَ ٱلْفَوْزُ ٱلْكَبِيرُ
Hakika walio amini na wakatenda mema watapata Bustani zenye mito ipitayo kati yake. Huko ndiko kufuzu kukubwa.
إِنَّ بَطْشَ رَبِّكَ لَشَدِيدٌ
Hakika kutesa kwa Mola wako Mlezi ni kukali.
إِنَّهُۥ هُوَ يُبْدِئُ وَيُعِيدُ
Yeye ndiye anaye anzisha na ndiye anaye rejeza tena,
وَهُوَ ٱلْغَفُورُ ٱلْوَدُودُ
Naye ni Mwenye kusamehe, Mwenye mapenzi,
ذُو ٱلْعَرْشِ ٱلْمَجِيدُ
Mwenye Kiti cha Enzi, Mtukufu,
فَعَّالٌۭ لِّمَا يُرِيدُ
Atendaye ayatakayo.
هَلْ أَتَىٰكَ حَدِيثُ ٱلْجُنُودِ
Je! Zimekuwasilia khabari za majeshi?
فِرْعَوْنَ وَثَمُودَ
Ya Firauni na Thamudi?
بَلِ ٱلَّذِينَ كَفَرُوا۟ فِى تَكْذِيبٍۢ
Lakini walio kufuru wamo katika kukadhibisha.
وَٱللَّهُ مِن وَرَآئِهِم مُّحِيطٌۢ
Na Mwenyezi Mungu nyuma yao amewazunguka.
بَلْ هُوَ قُرْءَانٌۭ مَّجِيدٌۭ
Bali hii ni Qur'ani tukufu
فِى لَوْحٍۢ مَّحْفُوظٍۭ
Katika Ubao Ulio Hifadhiwa.
Surah 86: At-Tariq — الطارق
وَٱلسَّمَآءِ وَٱلطَّارِقِ
Naapa kwa mbingu na Kinacho kuja usiku!
وَمَآ أَدْرَىٰكَ مَا ٱلطَّارِقُ
Na nini kitakacho kujuulisha ni nini hicho Kinacho kuja usiku?
ٱلنَّجْمُ ٱلثَّاقِبُ
Ni Nyota yenye mwanga mkali.
إِن كُلُّ نَفْسٍۢ لَّمَّا عَلَيْهَا حَافِظٌۭ
Hapana nafsi ila inayo mwangalizi.
فَلْيَنظُرِ ٱلْإِنسَٰنُ مِمَّ خُلِقَ
Hebu naajitazame mwanaadamu ameumbwa kwa kitu gani?
خُلِقَ مِن مَّآءٍۢ دَافِقٍۢ
Ameumbwa kwa maji yatokayo kwa kuchupa,
يَخْرُجُ مِنۢ بَيْنِ ٱلصُّلْبِ وَٱلتَّرَآئِبِ
Yatokayo baina ya mifupa ya mgongo na mbavu.
إِنَّهُۥ عَلَىٰ رَجْعِهِۦ لَقَادِرٌۭ
Hakika Yeye ana uweza wa kumrudisha.
يَوْمَ تُبْلَى ٱلسَّرَآئِرُ
Siku zitakapo dhihirishwa siri.
فَمَا لَهُۥ مِن قُوَّةٍۢ وَلَا نَاصِرٍۢ
Basi hatakuwa na nguvu wala msaidizi.
وَٱلسَّمَآءِ ذَاتِ ٱلرَّجْعِ
Naapa kwa mbingu yenye marejeo!
وَٱلْأَرْضِ ذَاتِ ٱلصَّدْعِ
Na kwa ardhi inayo pasuka!
إِنَّهُۥ لَقَوْلٌۭ فَصْلٌۭ
Hakika hii ni kauli ya kupambanua.
وَمَا هُوَ بِٱلْهَزْلِ
Wala si mzaha.
إِنَّهُمْ يَكِيدُونَ كَيْدًۭا
Hakika wao wanapanga mpango.
وَأَكِيدُ كَيْدًۭا
Na Mimi napanga mpango.
فَمَهِّلِ ٱلْكَٰفِرِينَ أَمْهِلْهُمْ رُوَيْدًۢا
Basi wape muhula makafiri - wape muhula pole pole.
Surah 87: Al-Ala — الأعلى
سَبِّحِ ٱسْمَ رَبِّكَ ٱلْأَعْلَى
Litakase jina la Mola wako Mlezi aliye juu kabisa,
ٱلَّذِى خَلَقَ فَسَوَّىٰ
Aliye umba, na akaweka sawa,
وَٱلَّذِى قَدَّرَ فَهَدَىٰ
Na ambaye amekadiria na akaongoa,
وَٱلَّذِىٓ أَخْرَجَ ٱلْمَرْعَىٰ
Na aliye otesha malisho,
فَجَعَلَهُۥ غُثَآءً أَحْوَىٰ
Kisha akayafanya makavu, meusi.
سَنُقْرِئُكَ فَلَا تَنسَىٰٓ
Tutakusomesha wala hutasahau,
إِلَّا مَا شَآءَ ٱللَّهُ ۚ إِنَّهُۥ يَعْلَمُ ٱلْجَهْرَ وَمَا يَخْفَىٰ
Ila akipenda Mwenyezi Mungu. Hakika Yeye anayajua yaliyo dhaahiri na yaliyo fichikana.
وَنُيَسِّرُكَ لِلْيُسْرَىٰ
Na tutakusahilishia yawe mepesi.
فَذَكِّرْ إِن نَّفَعَتِ ٱلذِّكْرَىٰ
Basi kumbusha, kama kukumbusha kunafaa.
سَيَذَّكَّرُ مَن يَخْشَىٰ
Atakumbuka mwenye kuogopa.
وَيَتَجَنَّبُهَا ٱلْأَشْقَى
Na atajitenga mbali nayo mpotovu,
ٱلَّذِى يَصْلَى ٱلنَّارَ ٱلْكُبْرَىٰ
Ambaye atauingia Moto mkubwa.
ثُمَّ لَا يَمُوتُ فِيهَا وَلَا يَحْيَىٰ
Tena humo hatakufa wala hawi hai.
قَدْ أَفْلَحَ مَن تَزَكَّىٰ
Hakika amekwisha fanikiwa aliye jitakasa.
وَذَكَرَ ٱسْمَ رَبِّهِۦ فَصَلَّىٰ
Na akakumbuka jina la Mola wake Mlezi, na akasali.
بَلْ تُؤْثِرُونَ ٱلْحَيَوٰةَ ٱلدُّنْيَا
Lakini nyinyi mnakhiari maisha ya dunia!
وَٱلْءَاخِرَةُ خَيْرٌۭ وَأَبْقَىٰٓ
Na Akhera ni bora na yenye kudumu zaidi.
إِنَّ هَٰذَا لَفِى ٱلصُّحُفِ ٱلْأُولَىٰ
Hakika haya yamo katika Vitabu vya mwanzo,
صُحُفِ إِبْرَٰهِيمَ وَمُوسَىٰ
Vitabu vya Ibrahimu na Musa.
Surah 88: Al-Ghashiyah — الغاشية
هَلْ أَتَىٰكَ حَدِيثُ ٱلْغَٰشِيَةِ
Je! Imekufikia khabari ya msiba wa kufudikiza?
وُجُوهٌۭ يَوْمَئِذٍ خَٰشِعَةٌ
Siku hiyo nyuso zitainama,
عَامِلَةٌۭ نَّاصِبَةٌۭ
Zikifanya kazi, nazo taabani.
تَصْلَىٰ نَارًا حَامِيَةًۭ
Ziingie katika Moto unao waka -
تُسْقَىٰ مِنْ عَيْنٍ ءَانِيَةٍۢ
Zikinyweshwa kutoka chemchem inayo chemka.
لَّيْسَ لَهُمْ طَعَامٌ إِلَّا مِن ضَرِيعٍۢ
Hawatakuwa na chakula isipo kuwa kichungu chenye miba.
لَّا يُسْمِنُ وَلَا يُغْنِى مِن جُوعٍۢ
Hakinenepeshi wala hakiondoi njaa.
وُجُوهٌۭ يَوْمَئِذٍۢ نَّاعِمَةٌۭ
Siku hiyo nyuso nyengine zitakuwa kunjufu.
لِّسَعْيِهَا رَاضِيَةٌۭ
Zitakuwa radhi kwa juhudi yao,
فِى جَنَّةٍ عَالِيَةٍۢ
Katika Bustani ya juu.
لَّا تَسْمَعُ فِيهَا لَٰغِيَةًۭ
Hawatasikia humo upuuzi.
فِيهَا عَيْنٌۭ جَارِيَةٌۭ
Humo imo chemchem inayo miminika.
فِيهَا سُرُرٌۭ مَّرْفُوعَةٌۭ
Humo vimo viti vilivyo nyanyuliwa,
وَأَكْوَابٌۭ مَّوْضُوعَةٌۭ
Na bilauri zilizo pangwa,
وَنَمَارِقُ مَصْفُوفَةٌۭ
Na matakia safu safu,
وَزَرَابِىُّ مَبْثُوثَةٌ
Na mazulia yaliyo tandikwa.
أَفَلَا يَنظُرُونَ إِلَى ٱلْإِبِلِ كَيْفَ خُلِقَتْ
Je! Hawamtazami ngamia jinsi alivyo umbwa?
وَإِلَى ٱلسَّمَآءِ كَيْفَ رُفِعَتْ
Na mbingu jinsi ilivyo inuliwa?
وَإِلَى ٱلْجِبَالِ كَيْفَ نُصِبَتْ
Na milima jinsi ilivyo thibitishwa?
وَإِلَى ٱلْأَرْضِ كَيْفَ سُطِحَتْ
Na ardhi jinsi ilivyo tandazwa?
فَذَكِّرْ إِنَّمَآ أَنتَ مُذَكِّرٌۭ
Basi kumbusha! Hakika wewe ni Mkumbushaji.
لَّسْتَ عَلَيْهِم بِمُصَيْطِرٍ
Wewe si mwenye kuwatawalia.
إِلَّا مَن تَوَلَّىٰ وَكَفَرَ
Lakini anaye rudi nyuma na kukataa,
فَيُعَذِّبُهُ ٱللَّهُ ٱلْعَذَابَ ٱلْأَكْبَرَ
Basi Mwenyezi Mungu atamuadhibu kwa adhabu iliyo kubwa kabisa!
إِنَّ إِلَيْنَآ إِيَابَهُمْ
Hakika ni kwetu Sisi ndio marejeo yao.
ثُمَّ إِنَّ عَلَيْنَا حِسَابَهُم
Kisha hakika ni juu yetu Sisi hisabu yao!
Surah 89: Al-Fajr — الفجر
وَٱلْفَجْرِ
Naapa kwa alfajiri,
وَلَيَالٍ عَشْرٍۢ
Na kwa masiku kumi,
وَٱلشَّفْعِ وَٱلْوَتْرِ
Na kwa viwili viwili na kimoja kimoja,
وَٱلَّيْلِ إِذَا يَسْرِ
Na kwa usiku unapo pita,
هَلْ فِى ذَٰلِكَ قَسَمٌۭ لِّذِى حِجْرٍ
Je! Hapana katika haya kiapo kwa mwenye akili?
أَلَمْ تَرَ كَيْفَ فَعَلَ رَبُّكَ بِعَادٍ
Kwani hukuona jinsi Mola wako Mlezi alivyo wafanya kina A'di?
إِرَمَ ذَاتِ ٱلْعِمَادِ
Wa Iram, wenye majumba marefu?
ٱلَّتِى لَمْ يُخْلَقْ مِثْلُهَا فِى ٱلْبِلَٰدِ
Ambao haukuumbwa mfano wake katika nchi?
وَثَمُودَ ٱلَّذِينَ جَابُوا۟ ٱلصَّخْرَ بِٱلْوَادِ
Na Thamudi walio chonga majabali huko bondeni?
وَفِرْعَوْنَ ذِى ٱلْأَوْتَادِ
Na Firauni mwenye vigingi?
ٱلَّذِينَ طَغَوْا۟ فِى ٱلْبِلَٰدِ
Ambao walifanya jeuri katika nchi?
فَأَكْثَرُوا۟ فِيهَا ٱلْفَسَادَ
Wakakithirisha humo ufisadi?
فَصَبَّ عَلَيْهِمْ رَبُّكَ سَوْطَ عَذَابٍ
Basi Mola wako Mlezi aliwapiga mjeledi wa adhabu.
إِنَّ رَبَّكَ لَبِٱلْمِرْصَادِ
Hakika Mola wako Mlezi yupo kwenye mavizio anawavizia.
فَأَمَّا ٱلْإِنسَٰنُ إِذَا مَا ٱبْتَلَىٰهُ رَبُّهُۥ فَأَكْرَمَهُۥ وَنَعَّمَهُۥ فَيَقُولُ رَبِّىٓ أَكْرَمَنِ
Ama mtu anapo jaribiwa na Mola wake Mlezi, akamkirimu na akamneemesha, husema: Mola wangu Mlezi amenikirimu!
وَأَمَّآ إِذَا مَا ٱبْتَلَىٰهُ فَقَدَرَ عَلَيْهِ رِزْقَهُۥ فَيَقُولُ رَبِّىٓ أَهَٰنَنِ
Na ama anapo mjaribu akampunguzia riziki yake, husema: Mola wangu Mlezi amenitia unyonge!
كَلَّا ۖ بَل لَّا تُكْرِمُونَ ٱلْيَتِيمَ
Sivyo hivyo! Bali nyinyi hamuwakirimu mayatima,
وَلَا تَحَٰٓضُّونَ عَلَىٰ طَعَامِ ٱلْمِسْكِينِ
Wala hamhimizani kulisha masikini;
وَتَأْكُلُونَ ٱلتُّرَاثَ أَكْلًۭا لَّمًّۭا
Na mnakula urithi kwa ulaji wa pupa,
وَتُحِبُّونَ ٱلْمَالَ حُبًّۭا جَمًّۭا
Na mnapenda mali pendo la kupita kiasi.
كَلَّآ إِذَا دُكَّتِ ٱلْأَرْضُ دَكًّۭا دَكًّۭا
Sivyo hivyo! Itakapo vunjwa ardhi vipande vipande,
وَجَآءَ رَبُّكَ وَٱلْمَلَكُ صَفًّۭا صَفًّۭا
Na akaja Mola wako Mlezi na Malaika safu safu,
وَجِا۟ىٓءَ يَوْمَئِذٍۭ بِجَهَنَّمَ ۚ يَوْمَئِذٍۢ يَتَذَكَّرُ ٱلْإِنسَٰنُ وَأَنَّىٰ لَهُ ٱلذِّكْرَىٰ
Na ikaletwa Jahannamu siku hiyo, siku hiyo mtu atakumbuka! Lakini kukumbuka huko kutamfaa nini?
يَقُولُ يَٰلَيْتَنِى قَدَّمْتُ لِحَيَاتِى
Atasema: Laiti ningeli jitangulizia kwa uhai wangu!
فَيَوْمَئِذٍۢ لَّا يُعَذِّبُ عَذَابَهُۥٓ أَحَدٌۭ
Basi siku hiyo hataadhibu yeyote namna ya kuadhibu kwake.
وَلَا يُوثِقُ وَثَاقَهُۥٓ أَحَدٌۭ
Wala hatafunga yeyote kama kufunga kwake.
يَٰٓأَيَّتُهَا ٱلنَّفْسُ ٱلْمُطْمَئِنَّةُ
Ewe nafsi iliyo tua!
ٱرْجِعِىٓ إِلَىٰ رَبِّكِ رَاضِيَةًۭ مَّرْضِيَّةًۭ
Rejea kwa Mola wako Mlezi umeridhika, na umemridhisha.
فَٱدْخُلِى فِى عِبَٰدِى
Basi ingia miongoni mwa waja wangu,
وَٱدْخُلِى جَنَّتِى
Na ingia katika Pepo yangu.
Surah 90: Al-Balad — البلد
لَآ أُقْسِمُ بِهَٰذَا ٱلْبَلَدِ
Naapa kwa Mji huu!
وَأَنتَ حِلٌّۢ بِهَٰذَا ٱلْبَلَدِ
Nawe unaukaa Mji huu.
وَوَالِدٍۢ وَمَا وَلَدَ
Na naapa kwa mzazi na alicho kizaa.
لَقَدْ خَلَقْنَا ٱلْإِنسَٰنَ فِى كَبَدٍ
Hakika tumemuumba mtu katika taabu.
أَيَحْسَبُ أَن لَّن يَقْدِرَ عَلَيْهِ أَحَدٌۭ
Ati anadhani hapana yeyote ataye muweza?
يَقُولُ أَهْلَكْتُ مَالًۭا لُّبَدًا
Anasema: Nimeteketeza chungu ya mali.
أَيَحْسَبُ أَن لَّمْ يَرَهُۥٓ أَحَدٌ
Ati anadhani ya kuwa hapana yeyote anaye mwona?
أَلَمْ نَجْعَل لَّهُۥ عَيْنَيْنِ
Kwani hatukumpa macho mawili?
وَلِسَانًۭا وَشَفَتَيْنِ
Na ulimi, na midomo miwili?
وَهَدَيْنَٰهُ ٱلنَّجْدَيْنِ
Na tukambainishia zote njia mbili?
فَلَا ٱقْتَحَمَ ٱلْعَقَبَةَ
Lakini hakujitoma kwenye njia ya vikwazo vya milimani.
وَمَآ أَدْرَىٰكَ مَا ٱلْعَقَبَةُ
Na nini kitakujuvya ni nini njia ya vikwazo vya milimani?
فَكُّ رَقَبَةٍ
Kumkomboa mtumwa;
أَوْ إِطْعَٰمٌۭ فِى يَوْمٍۢ ذِى مَسْغَبَةٍۢ
Au kumlisha siku ya njaa
يَتِيمًۭا ذَا مَقْرَبَةٍ
Yatima aliye jamaa,
أَوْ مِسْكِينًۭا ذَا مَتْرَبَةٍۢ
Au masikini aliye vumbini.
ثُمَّ كَانَ مِنَ ٱلَّذِينَ ءَامَنُوا۟ وَتَوَاصَوْا۟ بِٱلصَّبْرِ وَتَوَاصَوْا۟ بِٱلْمَرْحَمَةِ
Tena awe miongoni mwa walio amini na wakausiana kusubiri na wakausiana kuhurumiana.
أُو۟لَٰٓئِكَ أَصْحَٰبُ ٱلْمَيْمَنَةِ
Hao ndio watu wa kheri wa kuliani.
وَٱلَّذِينَ كَفَرُوا۟ بِـَٔايَٰتِنَا هُمْ أَصْحَٰبُ ٱلْمَشْـَٔمَةِ
Lakini walio zikataa Ishara zetu, hao ndio watu wa shari wa kushotoni.
عَلَيْهِمْ نَارٌۭ مُّؤْصَدَةٌۢ
Juu yao utakuwa Moto ulio fungiwa kila upande.
Surah 91: Ash-Shams — الشمس
وَٱلشَّمْسِ وَضُحَىٰهَا
Naapa kwa jua na mwangaza wake!
وَٱلْقَمَرِ إِذَا تَلَىٰهَا
Na kwa mwezi unapo lifuatia!
وَٱلنَّهَارِ إِذَا جَلَّىٰهَا
Na kwa mchana unapo lidhihirisha!
وَٱلَّيْلِ إِذَا يَغْشَىٰهَا
Na kwa usiku unapo lifunika!
وَٱلسَّمَآءِ وَمَا بَنَىٰهَا
Na kwa mbingu na kwa aliye ijenga!
وَٱلْأَرْضِ وَمَا طَحَىٰهَا
Na kwa ardhi na kwa aliye itandaza!
وَنَفْسٍۢ وَمَا سَوَّىٰهَا
Na kwa nafsi na kwa aliye itengeneza!
فَأَلْهَمَهَا فُجُورَهَا وَتَقْوَىٰهَا
Kisha akaifahamisha uovu wake na wema wake,
قَدْ أَفْلَحَ مَن زَكَّىٰهَا
Hakika amefanikiwa aliye itakasa,
وَقَدْ خَابَ مَن دَسَّىٰهَا
Na hakika amekhasiri aliye iviza.
كَذَّبَتْ ثَمُودُ بِطَغْوَىٰهَآ
Kina Thamudi walikadhibisha kwa sababu ya upotofu wao,
إِذِ ٱنۢبَعَثَ أَشْقَىٰهَا
Alipo simama mwovu wao mkubwa,
فَقَالَ لَهُمْ رَسُولُ ٱللَّهِ نَاقَةَ ٱللَّهِ وَسُقْيَٰهَا
Hapo Mtume wa Mwenyezi Mungu alipo waambia: Huyu ni ngamia wa Mwenyezi Mungu, mwacheni anywe maji fungu lake.
فَكَذَّبُوهُ فَعَقَرُوهَا فَدَمْدَمَ عَلَيْهِمْ رَبُّهُم بِذَنۢبِهِمْ فَسَوَّىٰهَا
Lakini walimkadhibisha na wakamchinja ngamia, kwa hivyo Mola wao Mlezi aliwaangamiza kwa sababu ya dhambi zao na akawafuta kabisa.
وَلَا يَخَافُ عُقْبَٰهَا
Wala Yeye haogopi matokeo yake.
Surah 92: Al-Lail — الليل
وَٱلَّيْلِ إِذَا يَغْشَىٰ
Naapa kwa usiku unapo funika!
وَٱلنَّهَارِ إِذَا تَجَلَّىٰ
Na mchana unapo dhihiri!
وَمَا خَلَقَ ٱلذَّكَرَ وَٱلْأُنثَىٰٓ
Na kwa Aliye umba dume na jike!
إِنَّ سَعْيَكُمْ لَشَتَّىٰ
Hakika juhudi zenu bila ya shaka ni mbali mbali.
فَأَمَّا مَنْ أَعْطَىٰ وَٱتَّقَىٰ
Ama mwenye kutoa na akamchamngu,
وَصَدَّقَ بِٱلْحُسْنَىٰ
Na akaliwafiki lilio jema,
فَسَنُيَسِّرُهُۥ لِلْيُسْرَىٰ
Tutamsahilishia yawe mepesi.
وَأَمَّا مَنۢ بَخِلَ وَٱسْتَغْنَىٰ
Na ama mwenye kufanya ubakhili, na asiwe na haja ya wenzake,
وَكَذَّبَ بِٱلْحُسْنَىٰ
Na akakanusha lilio jema,
فَسَنُيَسِّرُهُۥ لِلْعُسْرَىٰ
Tutamsahilishia yawe mazito!
وَمَا يُغْنِى عَنْهُ مَالُهُۥٓ إِذَا تَرَدَّىٰٓ
Na mali yake yatamfaa nini atapo kuwa anadidimia?
إِنَّ عَلَيْنَا لَلْهُدَىٰ
Hakika ni juu yetu kuonyesha uwongofu.
وَإِنَّ لَنَا لَلْءَاخِرَةَ وَٱلْأُولَىٰ
Na hakika ni yetu Sisi Akhera na dunia.
فَأَنذَرْتُكُمْ نَارًۭا تَلَظَّىٰ
Basi nakuonyeni na Moto unao waka!
لَا يَصْلَىٰهَآ إِلَّا ٱلْأَشْقَى
Hatauingia ila mwovu kabisa!
ٱلَّذِى كَذَّبَ وَتَوَلَّىٰ
Anaye kadhibisha na kupa mgongo.
وَسَيُجَنَّبُهَا ٱلْأَتْقَى
Na mchamngu ataepushwa nao,
ٱلَّذِى يُؤْتِى مَالَهُۥ يَتَزَكَّىٰ
Ambaye hutoa mali yake kwa ajili ya kujitakasa.
وَمَا لِأَحَدٍ عِندَهُۥ مِن نِّعْمَةٍۢ تُجْزَىٰٓ
Na wala si kwa kuwa yupo yeyote aliye mfanyia hisani ndio anamlipa.
إِلَّا ٱبْتِغَآءَ وَجْهِ رَبِّهِ ٱلْأَعْلَىٰ
Ila ni kutaka radhi ya Mola wake Mlezi aliye juu kabisa.
وَلَسَوْفَ يَرْضَىٰ
Naye atakuja ridhika!
Surah 93: Ad-Duha — الضحى
وَٱلضُّحَىٰ
Naapa kwa mchana!
وَٱلَّيْلِ إِذَا سَجَىٰ
Na kwa usiku unapo tanda!
مَا وَدَّعَكَ رَبُّكَ وَمَا قَلَىٰ
Mola wako Mlezi hakukuacha, wala hakukasirika nawe.
وَلَلْءَاخِرَةُ خَيْرٌۭ لَّكَ مِنَ ٱلْأُولَىٰ
Na bila ya shaka wakati ujao utakuwa bora kwako kuliko ulio tangulia.
وَلَسَوْفَ يُعْطِيكَ رَبُّكَ فَتَرْضَىٰٓ
Na Mola wako Mlezi atakupa mpaka uridhike.
أَلَمْ يَجِدْكَ يَتِيمًۭا فَـَٔاوَىٰ
Kwani hakukukuta yatima akakupa makaazi?
وَوَجَدَكَ ضَآلًّۭا فَهَدَىٰ
Na akakukuta umepotea akakuongoa?
وَوَجَدَكَ عَآئِلًۭا فَأَغْنَىٰ
Akakukuta mhitaji akakutosheleza?
فَأَمَّا ٱلْيَتِيمَ فَلَا تَقْهَرْ
Basi yatima usimwonee!
وَأَمَّا ٱلسَّآئِلَ فَلَا تَنْهَرْ
Na anaye omba au kuuliza usimkaripie!
وَأَمَّا بِنِعْمَةِ رَبِّكَ فَحَدِّثْ
Na neema za Mola wako Mlezi zisimlie.
Surah 94: Ash-Sharh — الشرح
أَلَمْ نَشْرَحْ لَكَ صَدْرَكَ
Hatukukunjulia kifua chako?
وَوَضَعْنَا عَنكَ وِزْرَكَ
Na tukakuondolea mzigo wako,
ٱلَّذِىٓ أَنقَضَ ظَهْرَكَ
Ulio vunja mgongo wako?
وَرَفَعْنَا لَكَ ذِكْرَكَ
Na tukakunyanyulia utajo wako?
فَإِنَّ مَعَ ٱلْعُسْرِ يُسْرًا
Basi kwa hakika pamoja na uzito upo wepesi,
إِنَّ مَعَ ٱلْعُسْرِ يُسْرًۭا
Hakika pamoja na uzito upo wepesi.
فَإِذَا فَرَغْتَ فَٱنصَبْ
Na ukipata faragha, fanya juhudi.
وَإِلَىٰ رَبِّكَ فَٱرْغَب
Na Mola wako Mlezi ndio mshughulikie.
Surah 95: At-Tin — التين
وَٱلتِّينِ وَٱلزَّيْتُونِ
Naapa kwa tini na zaituni!
وَطُورِ سِينِينَ
Na kwa Mlima wa Sinai!
وَهَٰذَا ٱلْبَلَدِ ٱلْأَمِينِ
Na kwa mji huu wenye amani!
لَقَدْ خَلَقْنَا ٱلْإِنسَٰنَ فِىٓ أَحْسَنِ تَقْوِيمٍۢ
Bila ya shaka tumemuumba mtu kwa umbo lilio bora kabisa.
ثُمَّ رَدَدْنَٰهُ أَسْفَلَ سَٰفِلِينَ
Kisha tukamrudisha kuwa chini kuliko walio chini!
إِلَّا ٱلَّذِينَ ءَامَنُوا۟ وَعَمِلُوا۟ ٱلصَّٰلِحَٰتِ فَلَهُمْ أَجْرٌ غَيْرُ مَمْنُونٍۢ
Lakini wale walio amini na wakatenda mema, hao watapata ujira usio kwisha.
فَمَا يُكَذِّبُكَ بَعْدُ بِٱلدِّينِ
Basi ni kipi baadaye kitacho kukukadhibishia malipo?
أَلَيْسَ ٱللَّهُ بِأَحْكَمِ ٱلْحَٰكِمِينَ
Kwani Mwenyezi Mungu si muadilifu kuliko mahakimu wote?
Surah 96: Al-Alaq — العلق
ٱقْرَأْ بِٱسْمِ رَبِّكَ ٱلَّذِى خَلَقَ
Soma kwa jina la Mola wako Mlezi aliye umba,
خَلَقَ ٱلْإِنسَٰنَ مِنْ عَلَقٍ
Amemuumba binaadamu kwa tone la damu,
ٱقْرَأْ وَرَبُّكَ ٱلْأَكْرَمُ
Soma! Na Mola wako Mlezi ni Karimu kushinda wote!
ٱلَّذِى عَلَّمَ بِٱلْقَلَمِ
Ambaye amefundisha kwa kalamu.
عَلَّمَ ٱلْإِنسَٰنَ مَا لَمْ يَعْلَمْ
Kamfundisha mtu aliyo kuwa hayajui.
كَلَّآ إِنَّ ٱلْإِنسَٰنَ لَيَطْغَىٰٓ
Kwani! Hakika mtu bila ya shaka huwa jeuri
أَن رَّءَاهُ ٱسْتَغْنَىٰٓ
Akijiona katajirika.
إِنَّ إِلَىٰ رَبِّكَ ٱلرُّجْعَىٰٓ
Hakika kwa Mola wako Mlezi ndio marejeo.
أَرَءَيْتَ ٱلَّذِى يَنْهَىٰ
Umemwona yule anaye mkataza
عَبْدًا إِذَا صَلَّىٰٓ
Mja anapo sali?
أَرَءَيْتَ إِن كَانَ عَلَى ٱلْهُدَىٰٓ
Umeona kama yeye yuko juu ya uwongofu?
أَوْ أَمَرَ بِٱلتَّقْوَىٰٓ
Au anaamrisha uchamngu?
أَرَءَيْتَ إِن كَذَّبَ وَتَوَلَّىٰٓ
Umeona kama yeye akikanusha na anarudi nyuma?
أَلَمْ يَعْلَم بِأَنَّ ٱللَّهَ يَرَىٰ
Hajui ya kwamba Mwenyezi Mungu anaona?
كَلَّا لَئِن لَّمْ يَنتَهِ لَنَسْفَعًۢا بِٱلنَّاصِيَةِ
Kwani! Kama haachi, tutamkokota kwa shungi la nywele!
نَاصِيَةٍۢ كَٰذِبَةٍ خَاطِئَةٍۢ
Shungi la uwongo, lenye makosa!
فَلْيَدْعُ نَادِيَهُۥ
Basi na awaite wenzake!
سَنَدْعُ ٱلزَّبَانِيَةَ
Nasi tutawaita Mazabania!
كَلَّا لَا تُطِعْهُ وَٱسْجُدْ وَٱقْتَرِب ۩
Hasha! Usimt'ii! Nawe sujudu na ujongee!
Surah 97: Al-Qadr — القدر
إِنَّآ أَنزَلْنَٰهُ فِى لَيْلَةِ ٱلْقَدْرِ
Hakika Sisi tumeiteremsha Qur'ani katika Laylatul Qadri, Usiku wa Cheo Kitukufu.
وَمَآ أَدْرَىٰكَ مَا لَيْلَةُ ٱلْقَدْرِ
Na nini kitacho kujuulisha nini Laylatul Qadri?
لَيْلَةُ ٱلْقَدْرِ خَيْرٌۭ مِّنْ أَلْفِ شَهْرٍۢ
Laylatul Qadri ni bora kuliko miezi elfu.
تَنَزَّلُ ٱلْمَلَٰٓئِكَةُ وَٱلرُّوحُ فِيهَا بِإِذْنِ رَبِّهِم مِّن كُلِّ أَمْرٍۢ
Huteremka Malaika na Roho katika usiku huo kwa idhini ya Mola wao Mlezi kwa kila jambo.
سَلَٰمٌ هِىَ حَتَّىٰ مَطْلَعِ ٱلْفَجْرِ
Amani usiku huo mpaka mapambazuko ya alfajiri.
Surah 98: Al-Bayinah — البينة
لَمْ يَكُنِ ٱلَّذِينَ كَفَرُوا۟ مِنْ أَهْلِ ٱلْكِتَٰبِ وَٱلْمُشْرِكِينَ مُنفَكِّينَ حَتَّىٰ تَأْتِيَهُمُ ٱلْبَيِّنَةُ
Hawakuwa walio kufuru miongoni mwa Watu wa Kitabu na washirikina waache walio nayo mpaka iwajie bayana,
رَسُولٌۭ مِّنَ ٱللَّهِ يَتْلُوا۟ صُحُفًۭا مُّطَهَّرَةًۭ
Yaani Mtume aliye toka kwa Mwenyezi Mungu anaye wasomea kurasa zilizo takasika,
فِيهَا كُتُبٌۭ قَيِّمَةٌۭ
Ndani yake mna maandiko yaliyo nyooka.
وَمَا تَفَرَّقَ ٱلَّذِينَ أُوتُوا۟ ٱلْكِتَٰبَ إِلَّا مِنۢ بَعْدِ مَا جَآءَتْهُمُ ٱلْبَيِّنَةُ
Wala hawakufarikiana walio pewa Kitabu ila baada ya kuwajia hiyo bayana.
وَمَآ أُمِرُوٓا۟ إِلَّا لِيَعْبُدُوا۟ ٱللَّهَ مُخْلِصِينَ لَهُ ٱلدِّينَ حُنَفَآءَ وَيُقِيمُوا۟ ٱلصَّلَوٰةَ وَيُؤْتُوا۟ ٱلزَّكَوٰةَ ۚ وَذَٰلِكَ دِينُ ٱلْقَيِّمَةِ
Nao hawakuamrishwa kitu ila wamuabudu Mwenyezi Mungu kwa kumtakasia Dini, wawe waongofu, na washike Sala, na watoe Zaka. Na hiyo ndiyo Dini madhubuti.
إِنَّ ٱلَّذِينَ كَفَرُوا۟ مِنْ أَهْلِ ٱلْكِتَٰبِ وَٱلْمُشْرِكِينَ فِى نَارِ جَهَنَّمَ خَٰلِدِينَ فِيهَآ ۚ أُو۟لَٰٓئِكَ هُمْ شَرُّ ٱلْبَرِيَّةِ
Hakika walio kufuru miongoni mwa Watu wa Kitabu na washirikina wataingia katika Moto wa Jahannamu wadumu milele humo. Hao ndio viumbe waovu kabisa.
إِنَّ ٱلَّذِينَ ءَامَنُوا۟ وَعَمِلُوا۟ ٱلصَّٰلِحَٰتِ أُو۟لَٰٓئِكَ هُمْ خَيْرُ ٱلْبَرِيَّةِ
Hakika walio amini na wakatenda mema, hao ndio bora wa viumbe.
جَزَآؤُهُمْ عِندَ رَبِّهِمْ جَنَّٰتُ عَدْنٍۢ تَجْرِى مِن تَحْتِهَا ٱلْأَنْهَٰرُ خَٰلِدِينَ فِيهَآ أَبَدًۭا ۖ رَّضِىَ ٱللَّهُ عَنْهُمْ وَرَضُوا۟ عَنْهُ ۚ ذَٰلِكَ لِمَنْ خَشِىَ رَبَّهُۥ
Malipo yao kwa Mola wao Mlezi ni Bustani za daima, zipitazo mito kati yake. Wakae humo milele. Mwenyezi Mungu yu radhi nao, na wao waradhi naye. Hayo ni kwa anaye mwogopa Mola wake Mlezi.
Surah 99: Az-Zalzalah — الزلزلة
إِذَا زُلْزِلَتِ ٱلْأَرْضُ زِلْزَالَهَا
Itakapo tetemeshwa ardhi kwa mtetemeko wake!
وَأَخْرَجَتِ ٱلْأَرْضُ أَثْقَالَهَا
Na itakapo toa ardhi mizigo yake!
وَقَالَ ٱلْإِنسَٰنُ مَا لَهَا
Na mtu akasema: Ina nini?
يَوْمَئِذٍۢ تُحَدِّثُ أَخْبَارَهَا
Siku hiyo itahadithia khabari zake.
بِأَنَّ رَبَّكَ أَوْحَىٰ لَهَا
Kwa sababu Mola wake Mlezi ameifunulia!
يَوْمَئِذٍۢ يَصْدُرُ ٱلنَّاسُ أَشْتَاتًۭا لِّيُرَوْا۟ أَعْمَٰلَهُمْ
Siku hiyo watu watatoka kwa mfarakano wakaonyweshwe vitendo vyao!
فَمَن يَعْمَلْ مِثْقَالَ ذَرَّةٍ خَيْرًۭا يَرَهُۥ
Basi anaye tenda chembe ya wema, atauona!
وَمَن يَعْمَلْ مِثْقَالَ ذَرَّةٍۢ شَرًّۭا يَرَهُۥ
Na anaye tenda chembe ya uovu atauona!
Surah 100: Al-Adiyat — العاديات
وَٱلْعَٰدِيَٰتِ ضَبْحًۭا
Naapa kwa farasi wendao mbio wakipumua,
فَٱلْمُورِيَٰتِ قَدْحًۭا
Na wakitoa moto kwa kupiga kwato zao chini,
فَٱلْمُغِيرَٰتِ صُبْحًۭا
Wakishambulia wakati wa asubuhi,
فَأَثَرْنَ بِهِۦ نَقْعًۭا
Huku wakitimua vumbi,
فَوَسَطْنَ بِهِۦ جَمْعًا
Na wakijitoma kati ya kundi,
إِنَّ ٱلْإِنسَٰنَ لِرَبِّهِۦ لَكَنُودٌۭ
Hakika mwanaadamu ni mtovu wa fadhila kwa Mola wake Mlezi!
وَإِنَّهُۥ عَلَىٰ ذَٰلِكَ لَشَهِيدٌۭ
Na hakika yeye mwenyewe bila ya shaka ni shahidi wa hayo!
وَإِنَّهُۥ لِحُبِّ ٱلْخَيْرِ لَشَدِيدٌ
Naye hakika bila ya shaka ana nguvu za kupenda mali!
۞ أَفَلَا يَعْلَمُ إِذَا بُعْثِرَ مَا فِى ٱلْقُبُورِ
Kwani hajui watakapo fufuliwa waliomo makaburini?
وَحُصِّلَ مَا فِى ٱلصُّدُورِ
Na yakakusanywa yaliomo vifuani?
إِنَّ رَبَّهُم بِهِمْ يَوْمَئِذٍۢ لَّخَبِيرٌۢ
Kuwa hakika Mola wao Mlezi siku hiyo bila ya shaka atakuwa na khabari zao wote!
Surah 101: Al-Qariah — القارعة
ٱلْقَارِعَةُ
Inayo gonga!
مَا ٱلْقَارِعَةُ
Nini Inayo gonga?
وَمَآ أَدْرَىٰكَ مَا ٱلْقَارِعَةُ
Na nini kitacho kujuilisha nini Inayo gonga?
يَوْمَ يَكُونُ ٱلنَّاسُ كَٱلْفَرَاشِ ٱلْمَبْثُوثِ
Siku ambayo watu watakuwa kama nondo walio tawanyika;
وَتَكُونُ ٱلْجِبَالُ كَٱلْعِهْنِ ٱلْمَنفُوشِ
Na milima itakuwa kama sufi zilizo chambuliwa!
فَأَمَّا مَن ثَقُلَتْ مَوَٰزِينُهُۥ
Basi yule ambaye mizani yake itakuwa nzito,
فَهُوَ فِى عِيشَةٍۢ رَّاضِيَةٍۢ
Huyo atakuwa katika maisha ya kupendeza.
وَأَمَّا مَنْ خَفَّتْ مَوَٰزِينُهُۥ
Na yule ambaye mizani yake itakuwa khafifu,
فَأُمُّهُۥ هَاوِيَةٌۭ
Huyo maskani yake yatakuwa Moto wa Hawiya!
وَمَآ أَدْرَىٰكَ مَا هِيَهْ
Na nini kitacho kujuilisha nini hiyo?
نَارٌ حَامِيَةٌۢ
Ni Moto mkali!
Surah 102: Al-Takathur — التكاثر
أَلْهَىٰكُمُ ٱلتَّكَاثُرُ
Kumekushughulisheni kutafuta wingi,
حَتَّىٰ زُرْتُمُ ٱلْمَقَابِرَ
Mpaka mje makaburini!
كَلَّا سَوْفَ تَعْلَمُونَ
Sivyo hivyo! Mtakuja jua!
ثُمَّ كَلَّا سَوْفَ تَعْلَمُونَ
Tena sivyo hivyo! Mtakuja jua!
كَلَّا لَوْ تَعْلَمُونَ عِلْمَ ٱلْيَقِينِ
Sivyo hivyo! Lau mngeli jua kwa ujuzi wa yakini,
لَتَرَوُنَّ ٱلْجَحِيمَ
Basi bila ya shaka mtaiona Jahannamu!
ثُمَّ لَتَرَوُنَّهَا عَيْنَ ٱلْيَقِينِ
Tena, bila ya shaka, mtaiona kwa jicho la yakini.
ثُمَّ لَتُسْـَٔلُنَّ يَوْمَئِذٍ عَنِ ٱلنَّعِيمِ
Tena bila ya shaka mtaulizwa siku hiyo juu ya neema.
Surah 103: Al-Asr — العصر
وَٱلْعَصْرِ
Naapa kwa Zama!
إِنَّ ٱلْإِنسَٰنَ لَفِى خُسْرٍ
Hakika binaadamu bila ya shaka yumo katika khasara,
إِلَّا ٱلَّذِينَ ءَامَنُوا۟ وَعَمِلُوا۟ ٱلصَّٰلِحَٰتِ وَتَوَاصَوْا۟ بِٱلْحَقِّ وَتَوَاصَوْا۟ بِٱلصَّبْرِ
Ila wale walio amini, na wakatenda mema, na wakausiana kwa haki, na wakausiana kusubiri.
Surah 104: Al-Humazah — الهمزة
وَيْلٌۭ لِّكُلِّ هُمَزَةٍۢ لُّمَزَةٍ
Ole wake kila safihi, msengenyaji!
ٱلَّذِى جَمَعَ مَالًۭا وَعَدَّدَهُۥ
Aliye kusanya mali na kuyahisabu.
يَحْسَبُ أَنَّ مَالَهُۥٓ أَخْلَدَهُۥ
Anadhani ya kuwa mali yake yatambakisha milele!
كَلَّا ۖ لَيُنۢبَذَنَّ فِى ٱلْحُطَمَةِ
Hasha! Atavurumishwa katika H'ut'ama.
وَمَآ أَدْرَىٰكَ مَا ٱلْحُطَمَةُ
Na nani atakujuvya ni nini H'ut'ama?
نَارُ ٱللَّهِ ٱلْمُوقَدَةُ
Moto wa Mwenyezi Mungu ulio washwa.
ٱلَّتِى تَطَّلِعُ عَلَى ٱلْأَفْـِٔدَةِ
Ambao unapanda nyoyoni.
إِنَّهَا عَلَيْهِم مُّؤْصَدَةٌۭ
Hakika huo utafungiwa nao
فِى عَمَدٍۢ مُّمَدَّدَةٍۭ
Kwenye nguzo zilio nyooshwa.
Surah 105: Al-Fil — الفيل
أَلَمْ تَرَ كَيْفَ فَعَلَ رَبُّكَ بِأَصْحَٰبِ ٱلْفِيلِ
Kwani hukuona jinsi Mola wako Mlezi alivyo watenda wale wenye tembo?
أَلَمْ يَجْعَلْ كَيْدَهُمْ فِى تَضْلِيلٍۢ
Kwani hakujaalia vitimbi vyao kuharibika?
وَأَرْسَلَ عَلَيْهِمْ طَيْرًا أَبَابِيلَ
Na akawapelekea ndege makundi kwa makundi,
تَرْمِيهِم بِحِجَارَةٍۢ مِّن سِجِّيلٍۢ
Wakiwatupia mawe ya udongo wa Motoni,
فَجَعَلَهُمْ كَعَصْفٍۢ مَّأْكُولٍۭ
Akawafanya kama majani yaliyo liwa!
Surah 106: Quraish — قريش
لِإِيلَٰفِ قُرَيْشٍ
Kwa walivyo zoea Maqureshi,
إِۦلَٰفِهِمْ رِحْلَةَ ٱلشِّتَآءِ وَٱلصَّيْفِ
Kuzoea kwao safari za siku za baridi na siku za joto.
فَلْيَعْبُدُوا۟ رَبَّ هَٰذَا ٱلْبَيْتِ
Basi nawamuabudu Mola Mlezi wa Nyumba hii,
ٱلَّذِىٓ أَطْعَمَهُم مِّن جُوعٍۢ وَءَامَنَهُم مِّنْ خَوْفٍۭ
Ambaye anawalisha wasipate njaa, na anawalinda na khofu.
Surah 107: Al-Ma'un — الماعون
أَرَءَيْتَ ٱلَّذِى يُكَذِّبُ بِٱلدِّينِ
Je! Umemwona anaye kadhibisha Malipo?
فَذَٰلِكَ ٱلَّذِى يَدُعُّ ٱلْيَتِيمَ
Huyo ndiye anaye msukuma yatima,
وَلَا يَحُضُّ عَلَىٰ طَعَامِ ٱلْمِسْكِينِ
Wala hahimizi kumlisha masikini.
فَوَيْلٌۭ لِّلْمُصَلِّينَ
Basi, ole wao wanao sali,
ٱلَّذِينَ هُمْ عَن صَلَاتِهِمْ سَاهُونَ
Ambao wanapuuza Sala zao;
ٱلَّذِينَ هُمْ يُرَآءُونَ
Ambao wanajionyesha,
وَيَمْنَعُونَ ٱلْمَاعُونَ
Nao huku wanazuia msaada.
Surah 108: Al-Kauthar — الكوثر
إِنَّآ أَعْطَيْنَٰكَ ٱلْكَوْثَرَ
Hakika tumekupa kheri nyingi.
فَصَلِّ لِرَبِّكَ وَٱنْحَرْ
Basi sali na uchinje kwa ajili ya Mola wako Mlezi.
إِنَّ شَانِئَكَ هُوَ ٱلْأَبْتَرُ
Hakika anaye kuchukia ndiye aliye mpungufu.
Surah 109: Al-Kafirun — الكافرون
قُلْ يَٰٓأَيُّهَا ٱلْكَٰفِرُونَ
Sema: Enyi makafiri!
لَآ أَعْبُدُ مَا تَعْبُدُونَ
Siabudu mnacho kiabudu;
وَلَآ أَنتُمْ عَٰبِدُونَ مَآ أَعْبُدُ
Wala nyinyi hamuabudu ninaye muabudu.
وَلَآ أَنَا۠ عَابِدٌۭ مَّا عَبَدتُّمْ
Wala sitaabudu mnacho abudu.
وَلَآ أَنتُمْ عَٰبِدُونَ مَآ أَعْبُدُ
Wala nyinyi hamuabudu ninaye muabudu.
لَكُمْ دِينُكُمْ وَلِىَ دِينِ
Nyinyi mna dini yenu, nami nina Dini yangu.
Surah 110: An-Nasr — النصر
إِذَا جَآءَ نَصْرُ ٱللَّهِ وَٱلْفَتْحُ
Itakapo kuja nusura ya Mwenyezi Mungu na ushindi,
وَرَأَيْتَ ٱلنَّاسَ يَدْخُلُونَ فِى دِينِ ٱللَّهِ أَفْوَاجًۭا
Na ukaona watu wanaingia katika Dini ya Mwenyezi Mungu kwa makundi,
فَسَبِّحْ بِحَمْدِ رَبِّكَ وَٱسْتَغْفِرْهُ ۚ إِنَّهُۥ كَانَ تَوَّابًۢا
Zitakase sifa za Mola wako Mlezi, na umwombe msamaha; hakika Yeye ndiye anaye pokea toba.
Surah 111: Al-Masad — المسد
تَبَّتْ يَدَآ أَبِى لَهَبٍۢ وَتَبَّ
Imeangamia mikono ya Abu Lahab, na yeye pia ameangamia.
مَآ أَغْنَىٰ عَنْهُ مَالُهُۥ وَمَا كَسَبَ
Hayatamfaa mali yake, wala alivyo vichuma.
سَيَصْلَىٰ نَارًۭا ذَاتَ لَهَبٍۢ
Atauingia Moto wenye mwako.
وَٱمْرَأَتُهُۥ حَمَّالَةَ ٱلْحَطَبِ
Na mkewe, mchukuzi wa kuni,
فِى جِيدِهَا حَبْلٌۭ مِّن مَّسَدٍۭ
Shingoni mwake iko kamba iliyo sokotwa.
Surah 112: Al-Ikhlas — الإخلاص
قُلْ هُوَ ٱللَّهُ أَحَدٌ
Sema: Yeye Mwenyezi Mungu ni wa pekee.
ٱللَّهُ ٱلصَّمَدُ
Mwenyezi Mungu Mkusudiwa.
لَمْ يَلِدْ وَلَمْ يُولَدْ
Hakuzaa wala hakuzaliwa.
وَلَمْ يَكُن لَّهُۥ كُفُوًا أَحَدٌۢ
Wala hana anaye fanana naye hata mmoja.
Surah 113: Al-Falaq — الفلق
قُلْ أَعُوذُ بِرَبِّ ٱلْفَلَقِ
Sema: Najikinga kwa Mola Mlezi wa mapambazuko,
مِن شَرِّ مَا خَلَقَ
Na shari ya alivyo viumba,
وَمِن شَرِّ غَاسِقٍ إِذَا وَقَبَ
Na shari ya giza la usiku liingiapo,
وَمِن شَرِّ ٱلنَّفَّٰثَٰتِ فِى ٱلْعُقَدِ
Na shari ya wanao pulizia mafundoni,
وَمِن شَرِّ حَاسِدٍ إِذَا حَسَدَ
Na shari ya hasidi anapo husudu.
Surah 114: An-Nas — الناس
قُلْ أَعُوذُ بِرَبِّ ٱلنَّاسِ
Sema: Ninajikinga kwa Mola Mlezi wa wanaadamu,
مَلِكِ ٱلنَّاسِ
Mfalme wa wanaadamu,
إِلَٰهِ ٱلنَّاسِ
Mungu wa wanaadamu,
مِن شَرِّ ٱلْوَسْوَاسِ ٱلْخَنَّاسِ
Na shari ya wasiwasi wa Shetani, Khannas,
ٱلَّذِى يُوَسْوِسُ فِى صُدُورِ ٱلنَّاسِ
Anaye tia wasiwasi katika vifua vya watu,
مِنَ ٱلْجِنَّةِ وَٱلنَّاسِ
Kutokana na majini na wanaadamu.